Jumanne, 9 Juni 2015

Yaliojili katika uzinduzi wa chawakama Chuo cha kumbukumbu ya Mwl. Nyerere





Viongozi wa chawakama tawi la mwalimu nyerere wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi prof H. Mwansoko wakati wa sherehe za uzinduzi wa chama hicho. kutoka kulia walio kaa ni rais mh Komanya wa pili ni makamu mkuu wa chuo mipango na fedha Dr Shawa wa tatu  mgeni rasmi prof H. Mwansoko ambaye Mkurugenzi wa lugha katika wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo. 4 ni mwenyekiti ndugu Christopher Anthony. na mwisho ni mkuu wa idara ya elimu ndugu Msolwa

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++


      LUMBA LUMBA KISWAHILI NA UKUZWE UZALENDO+
1.   CHAWAKAMA mjibari, niwajuza haki yenu,
    Natoa langu shauri, hii ni dhamana yenu,
    Moja ilahi kahari, mmefanya Chama chenu,
        Lumba lumba Kiswahili,  Naukuzwe uzalendo.

2.   Msingoje kusubiri,  kutendewa kazi zenu,
    Msinune mfikiri, fanyeni amuzi lenu,
    Ni kama mwajiathiri, kuzuiwa kasi yenu,
    Duri Dawiri na Zari, tuwapambe CHAWAKAMA,
     Lumba  lumba Kiswahili, naukuzwe uzalendo.

3.   Tumesimama majabari,  kutongoa wito wetu,
Tunaifanya dhamiri,  yasambae mambo yetu,
Chuo kiwe mshauri,  kikiwa mlezi wetu,
    Lumba lumba Kiswahili,  na ukuzwe uzalendo.

4.    Na katu msijibari,  Kiswahili lugha yetu,
Tamu isiyo shubiri,  nzuri mno ya kikwetu,
Teo ifungwe tayari,  kihodari kila utu,
    Vigelegele na shangwe,  Shangilia mashujaa.

5.   Mafunzo ya ikibari, yawe vitabuni mwetu,
Mmeapa kwa hiari, kuikuza lugha yetu,
    Yarabi na uibari, CHAWAKAMA ya wanetu,
    Tawi limefunguliwa, CHAWAKAMA ya Nyerere.

6.   Hongereni mashujaa, kufungua tawi lenu,
Akiba ya manufaa, itunzeni amana yenu,
Sichoki kuwa asaa, jahazi peleka kwenu,
Simameni wahadhiri, shangilia mashujaa,
     Lumba lumba Kiswahili, naukuzwe uzalendo.



7.   Mko wapi washairi,  Malenga manguli wetu,
   Tupokeeni mkiri,  msitucheke  wenzetu,
   Na hasa mtuamiri, hiki ni kiapo chetu,
       Fenella  wa  Mukangara,  twaomba pongezi zetu.




8.   Natamatisha shairi,  sina kinyongo na mtu,
Nimeeleza dhahiri,  Sijaficha hata kitu,
Kwa kweli mko tayari,  kulijenga bara letu,
     Lumba lumba Kiswahili, naukuzwe uzalendo.



Mtunzi wa Shairi ni Sikuzani wa Jalala (Nitendeje)
Limeruwazwa na kughaniwa na Hajjat Shani Kitogo (Sauti ya Asali)

Shairi limeimbwa siku ya sherehe ya uzinduzi wa Tawi la Chama cha Wanafunzi wa Kiswahili Afrika Mashariki (CHAWAKAMA), Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Tarehe 8/5/2015 katika Ukumbi wa Utamaduni.

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni