Jumanne, 6 Oktoba 2015

Nini tofauti ya Kiswahili SANIFU na FASAHA?

Kuongea/kuandika Kiswahili Fasaha ni ile jinsi unavyo andika au kuongea bila kukosea kutamka herufi mfano: Ukiandika Neno Barua (walaka) hapo umeandika au kutamka kiswahili fasaha, kinyume chake BALUA hili neno si Kiswahili fasaha japokuwa unaweza kueleweka.

Kiswahili Sanifu ni kiswahili kilichofanyiwa marekebisho kutoka lugha nyingine na kuingizwa kwenye lugha husika... mfano neno... password ni nywila, barua pepe (email) nk.

Kwa ufupi tunaweza kusema kuwa ufasaha na usanifu ni kiswahili kilicho tungiwa kanuni zinazokubalika kwenye uwanja wa taaluma ya lugha.

Punde: Soon, in a little while, presently

Punde si punde: Inatumika kwa kumaanisha: Baada ya muda mchache (soon, in a moment, Thereafter)

Punde kwa punde: Kidogo kidogo (little by little, gradually)

Hivi punde: Muda mchache, (Shortly)

Mifano:
  • Kiswahili: tulikuwa tunamngoja, na punde akaja.
  • English: we waited for him, and he soon came.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni